TAHADHARI: KONA HIZI ZA IYOVI NI KALI, DEREVA KUWA MAKINI, EPUSHA MAISHA YA ABIRIA







Wewe ni  dereva  wa basi la abiria ama gari  binafsi ? hebu  chukua  hatua ya  kupunguza ajali  leo kwa kujihadhari na  kona  hizi na Iyovi na Kitonga na  kona  nyingine kali kama  hizi nchini kwani maisha  yako ni  dhamani  kubwa na uhai  wake bado tunautamani.
 Vema  kuheshimu alama  za barabarani na  kuacha mbwembwe  uwapo  barabarani katika kona kali kama hizi.




 Katika kona  kama  hizi  zingatia  alama  za usalama  barabarani  usiwe na haraka  ya  kulipita gari la mbele.
Kulipita gari la mbele katika kona kama hizi ni hatari.
Hapa  ni eneo ambalo  watu 19  walipoteza maisha kwa fuso kugongana na basi na Nganga na kisha  kuwaka  moto uzembe  ukiwa ni wa dereva wa basi aliyetaka  kulipita gari la  mbele  katika  kona kali.
 
 Usilipite gari katika  kona kama hili.
 Alama  zote  za barabarani ni msaada kwa maisha  yako lazima  uziheshimu
 Kona  zote ni hatari kwa usalama  wako hivyo  usihame saiti  yako ili  kukimbia ajali.
 Lazima  unapotaka  kulipita gari la  mbele uwe una uwezo wa kuona mbali  zaidi ya mita  100 ama  zaidi.
 Dereva makini halipiti gari  la  mbele katika  kona
Kumbuka  ni  heri  kuchelewa  ukafika  salama  kuliko kuendesha kwa haraka na ukafika majeruhi ama maiti tambua Taifa  linakuhitaji familia  inakuhitaji na  wewe  dereva ni msaada wa abiria  wote katika gari lako  na  msaada wa maisha  yako jitambue ,watambue abiria  wako , jilinde utulinde  abiria  wako maisha  yako   ni yetu na uhai  wako ni tegemeo letu epuka ajali zingatia sheria  za barabarani. IMETOLEWA NA MATUKIODAIMABLOG