MWANAUME WA UGANDA AFUNGUKA: ZARI AMETOA MIMBA ZANGU 2






Hasira ya kibuti? Ubuyu kutoka nyumba ya jirani, Kampala nchini Uganda unaeleza kuwa mwanaume Farouk Sempala aliyewahi kuwa mpenzi wa mwandani wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ ameibuka na madai mazito kuwa mwanamama huyo alichoropoa mimba zake zaidi ya mbili.
Staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, akiwa na mpenzi wake Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady.
TUJIUNGE UGANDA
Katika mahojiano maalum na Gazeti la Red Pepper la nchini humo hivi karibuni, Sempala alifunguka kuwa alishtushwa na habari kuwa mwanadada huyo alikutana na Diamond kwenye ndege na kuanza projekti ambayo matokeo yake ni mimba.
MIMBA ZAIDI YA 2
Jamaa huyo alidai kuwa, wakati akiwa kwenye mapenzi na Zari baada ya mwanamama huyo kutengana na mumewe, Ivan Semwanga, alitoa mimba zake zaidi ya mbili hivyo anaamini kuwa hata hiyo ya Diamond anaweza kuichoropoa.Sempala alisema kuwa katika kipindi cha mapenzi yao, walikuwa hawatumii kinga hivyo Zari alikuwa akinasa mimba lakini akawa anachoropoa.
Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady akiwa na aliyekuwa mpenzi wake sempala.
AANIKA SIRI ZA NDANI
“Tulifanya ngono laivu tena mara nyingi tu bila kinga.



“Katika kufanya hivyo nilimpa mimba siyo mara moja wala mbili lakini alikuwa akizichoropoa.
“Kamwe Zari hakunipenda. Alichotaka ni kumuonesha tu Ivan (aliyekuwa mume wa Zari) kwamba alikuwa amepata mwanaume mwenye misuli,” alianika siri zao Sempala katika gazeti hilo.
AMECHUKUA HATUA GANI?
Alipoulizwa juu ya hatua alizochukua au anazotarajia kuzichukua kwa Zari, Sempala alisema hakuna hatua atakayochukua lakini ameamua kusema juu ya uchoropoaji huo wa mimba akiwa na wasiwasi kuwa huenda hata hiyo ya Diamond ataichoropoa hivyo achukue tahadhari.
GUMZO
Habari kutoka kwa chanzo chetu chenye maskani yake Chuo Kikuu cha Kampala (Kiu) nchini Uganda kililitonya Amani kwamba, baada ya habari hiyo kuingia mitaani iligeuka gumzo kubwa huku wengi wakieleza kuwa huenda Sempala ameamua kumchafua Zari kwa sababu mwanamama huyo alimpiga kibuti cha kihistoria.
“Yaani gumzo hapa Kampala ni habari hiyo ambayo imetoka kwa ukubwa kwenye ukurasa wa mbele wa gazeti.
“Unajua huyu Sempala bado kiroho kinamuuma. Kinachoonekana anatapatapa kwa sababu Zari alimpiga kibuti kibaya na cha ghafla kisha akanasa kwa Diamond,” kilisema chanzo hicho.
Zari na Sempala wakipozi kimahaba.
SEMPALA ACHUKIA UHUSIANO WA ZARI, DIAMOND
Kati ya watu wa mwanzo walioponda uhusiano wa Zari na Diamond ni Sempala ambaye alinukuliwa na vyombo vya habari nchini humo akisema kwamba hapendezwi kabisa na pea ya wawili hao.
Habari zilieleza kwamba Sempala ambaye anasifika kwa dili za mjini, anaonekana kutokuwa katika hali ya kawaida tangu alipopigwa chini na Zari mwaka jana hivyo kuchukuliwa kama anasema chochote kutokana na kuchanganyikiwa.
ZARI YUPO SAUZI
Juhudi za kumpata Zari ambaye ni mama wa watoto watatu akitarajia kupata wa nne, aliyeko nchini Afrika Kusini ’Sauzi’ ili kusikia upande wake juu ya sakata hilo, ziligonga mwamba hivyo zinaendelea.
Diamond alipotafutwa na kunyetishiwa ishu hiyo alisema kuwa hana la kusema na hawezi kushindana na midomo ya watu.
Source GPL