Stanbic Bank Yakwama Kutaja Majina ya Waliochota Pesa za Escrow Kwa Malumbesa na Rambo, Yatimua Wafanyakazi Kadhaa





Taarifa za ndani ya Stanbic zinadai kuwa benki hiyo imeshindwa kutaja majina ya waliochota mabilioni ya Escrow kwa Malumbesa na Rambo. Taarifa hizo zinadai kuwa, pamoja na kuwepo kwa nia hiyo, benki hiyo ilikumbana na vikwazo vya ndani na nje ya benki hiyo hadi kukubali kukaa kimya. Ilipangwa kuwa,majina ya waliochota mabilioni ya Escrow kupitia miamala ya Stanbic yangewekwa hadharani hadi kufikia Aprili 1,2015.




Hatahivyo, Stanbic inadaiwa kuwatimua kazi wafanyakazi mbalimbali waliohusishwa na miamala hiyo iliyokuwa na harufu na tuhuma za ufisadi. Wafanyakazi hao ni wa ngazi na kada mbalimbali ndani ya Stanbic. Huu ndiyo mwisho wa filamu ya kujulikana kwa waliochota mabilioni ya Escrow kwa lumbesa na rambo? Tujipe moyo!