Sitta awaonya wasafirishaji wa dawa za kulevya, Adai Sasa Wamebadili Mbinu na Amezigundua






Sitta
Waziri wa Uchukuzi Mhe. Samuel Sitta, amesema hatokubali kuona viwanja vya ndege nchini vinakuwa uchochoro wa kupitishia dawa za kulevya na kwamba atahakikisha usafirishaji wa dawa hizo nchini unakomeshwa kabisa.



Akizungumza katika mahojiano na East Africa Radio muda mfupi baada ya kuongelea maadhimisho ya siku ya kimataifa ya hali ya hewa, Waziri Sitta amesema hivi sasa wasafirishaji wa dawa hizo wamebadili mbinu na kuanza kutumia njia ya bahari baada ya ulinzi kuimarishwa katika viwanja vya ndege na katika maeneo ya mipakani.....