Kumbe uigizaji uliwahi kumletea mzozo Muhogo Mchungu kisa mke wa mtu? #Hekaheka---->>







IMG_3698Muigizaji mkongwe Muhogo Mchungu leo alikuwa mgeni kwenye LEO TENA mtu wangu.. kuhusu sanaa yake, wapi anapenda na wapi hapendi kuingiza.. Ishu ya kuigiza kama baba mwenye nyumba ndogo kumbe ni waandaaji wa filamu hizo wanapenda kumpanga kwenye nafasi hizo.




Akizungumzia Hekaheka ambayo iliwahi kukutana nayo kuna siku walienda Shinyanga kwenye michezo ya jadi kitaifa, akakutana na dada mmoja ambae alitaka kufanya filamu wakawa wanawasiliana.
Baadaye mume wa dada huyo alimtuhumu Muhogo kuwa na uhusiano na mpenzi wake baada ya kukuta message walizokuwa wanatumiana, japo alijaibu kumuelekea kuwa walikuwa kwenye majadiliano kuhusu filamu mwanaume huyo hakuelewa.
Kuhusu watu ambao anapenda kucheza nao filamu amesema anaelewana sana na Bi Staa kutokana na kwamba walianza wote sanaa.
Muhogo Mchungu amesema anaipenda sana tamthilia ya Fukuto na filamu ya Kigodoro.