WATANZANIA TUMPE SUPPORT MISS TANZANIA HAPPINESS WATIMANYWA KWENYE SHINDANO LA MISS WORLD 2014‏‎



 Happiness Watimanywa (20) aliyekuwa Redds Miss Tanzania 2013 sasa yuko jijini London Uingereza kwa ajili ya kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya Miss World 2014. 

Happiness ambaye kwa sasa anashikilia taji la Miss World Tanzania 2014 amesema ana kila sababu ya kurudisha taji nyumbani ikiwa watanzania watamuunga mkono kwa kusambaza video zake katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

"Hebu angalia uzuri wa taifa letu, amani, upendo na vivutio mbalimbali vya utalii. Hebu niangalie na mimi mwenyewe... tuna kila sababu ya kurudisha taji nyumbani." alisema Happiness Watimanywa

Shime shime watanzania, tumuunge mkono wa nyumbani kwa ku-retweet, ku-like na ku-share post zake mbalimbali kwa kutumia Hashtag #Happiness4MissWorld