Suarez akiwa na mchezaji mwenzake mara tu alipotoka zoezini na klabu ya Barecelona
In Summary
Kwa kuanzia, Suarez anaweza kucheza katika pambano
la kirafiki la leo Jumatatu la Barcelona dhidi ya Leon Guanajuato, hii
ni kwa mujibu wa mchambuzi wa masuala ya soka nchini Hispania, Guillem
Balague.
Kwa kuanzia, Suarez anaweza kucheza katika pambano
la kirafiki la leo Jumatatu la Barcelona dhidi ya Leon Guanajuato, hii
ni kwa mujibu wa mchambuzi wa masuala ya soka nchini Hispania, Guillem
Balague.
Suarez alifungiwa na Shirikisho la Kimataifa la
Vyama vya Soka (Fifa) kwenye Kombe la Dunia kule Brazil hivi karibuni
kwa kosa la kumng’ata beki wa timu ya taifa ya Italia, Georgio
Chiellini. Alikuwa akiichezea timu yake ya taifa ya Uruguay.
Matokeo yake, staa huyo wa zamani wa Liverpool
alifungiwa kucheza soka kwa miezi minne huku pia akifungiwa kuichezea
timu ya taifa ya Uruguay mechi tisa na pia akiambiwa asijishughulishe na
lolote kuhusu soka.
Hata hivyo, Alhamisi iliyopita mahakama ya masuala
ya kimichezo ilimruhusu Suarez kufanya mazoezi na Barcelona huku pia
ikidaiwa kuwa anaruhusiwa kucheza mechi zisizo za mashindano na timu
hiyo ya Catalunya.
Balague anaamini kwamba hukumu hiyo itawafurahisha
Suarez na Barcelona ambao wanaamini kwamba wanaweza kufanya ujanja
ujanja wa kumuweka fiti mchezaji huyo.
Mchambuzi huyo pia anaamini kuwa Barcelona inajipanga kumuandalia Suarez mechi nyingi za kirafiki.
“Naamini kuwa haikuwa sahihi kumzuia asifanye kazi
yake kabisa. Hakuweza hata kufanya mazoezi katika uwanja wa soka.
Nadhani atatambulishwa rasmi muda wowote kuanzia sasa hasa Jumatatu
(leo),” alisema.
“Kuna michuano ya Kombe la Gamper ambayo kwa
mujibu wa utamaduni wao inatumika kutambulisha wachezaji wao. Watacheza
na Leon na ni kitu wanachofanya kila mwaka. Kuna wazo la kumtumia
Suarez.
“Kumekuwapo na mawazo kwamba Barcelona inaweza pia
kuandaa mechi nyingi za kirafiki katika uwanja usio na mashabiki na
ambao utafungwa milango kwa ajili ya kumfanya acheze mechi nyingi za
kumweka fiti.
“Fifa pia bado haijaamua kama Suarez anaweza
kuruhusiwa kucheza mechi za kirafiki za Uruguay. Lakini kwa vyovyote
vile, lazima Barcelona na wanasheria wa Suarez watakuwa na furaha na
hukumu hii.”