Wananchi chukueni hatua za dharura!!!
====UPDATES====
- Tayari walioiba ripoti hiyo washaanza kukamatwa. Mohamed Mbaruk ndugu wa Prof. Muhongo amekamatwa na shehena ya ripoti hiyo iliyonyofolewa kurasa 56,57,59... Kwa sasa yupo kituo cha Polisi kati Dodoma na amewataja walio kwenye zoezi la kusambaza ripoti hiyo kuwa ni pamoja na mtu maarufu aitwae "Chifu Kiumbe" ambaye Jeshi la Polisi tayari wanamfuatilia kwa ukaribu usiku huu. Na mwisho amesema katumwa na wakubwa (mafisadi).
Sunday, November 23, 2014
RIPOTI YA CAG, PAC, INAYOHUSU SAKATA LA ESCROW YAIBIWA BUNGENI
Wakuu hali ya taharuki imeibuka baada ya kuibiwa na kunyofoa kurasa zenye ushahidi wote wa wizi na majina ya wezi wote.
Kurasa za 56,57,59... Zote zimenyofolewa, kibaya zaidi wezi hawa wameiba
kuanzia iliyopo Bunge kwa Kashilila, Kwa ofisi ya PAC, na ile ya CAG
huko Dar,Hali sasa inayoendelea ni kuwa ripoti iliyobaki isiyo na ushahidi wala
makali wezi hawa wamewagawia wabunge wa CCM na wananchi mtaani ili na
kuwaambia wajionee wenyewe ripoti haina mtu wakuwajibika.