Wakuu hali ya taharuki imeibuka baada ya kuibiwa na kunyofoa kurasa zenye ushahidi wote wa wizi na majina ya wezi wote.
Kurasa za 56,57,59... Zote zimenyofolewa, kibaya zaidi wezi hawa wameiba
kuanzia iliyopo Bunge kwa Kashilila, Kwa ofisi ya PAC, na ile ya CAG
huko Dar,Hali sasa inayoendelea ni kuwa ripoti iliyobaki isiyo na ushahidi wala
makali wezi hawa wamewagawia wabunge wa CCM na wananchi mtaani ili na
kuwaambia wajionee wenyewe ripoti haina mtu wakuwajibika.
Wananchi chukueni hatua za dharura!!!
====UPDATES====
- Tayari walioiba ripoti hiyo washaanza kukamatwa. Mohamed Mbaruk ndugu
wa Prof. Muhongo amekamatwa na shehena ya ripoti hiyo iliyonyofolewa
kurasa 56,57,59... Kwa sasa yupo kituo cha Polisi kati Dodoma na
amewataja walio kwenye zoezi la kusambaza ripoti hiyo kuwa ni pamoja na
mtu maarufu aitwae "Chifu Kiumbe" ambaye Jeshi la Polisi tayari
wanamfuatilia kwa ukaribu usiku huu. Na mwisho amesema katumwa na
wakubwa (mafisadi).
Taarifa ya (CAG) yakutwa ikisambazwa mitaani ikiwa imenyofolewa kurasa.
Taarifa ya mdhibiti na mkaguzi wa hesabu za serikali kuhusiana na kashfa
ya wizi wa bilioni 321 kwenye akaunti ya tegeta Escrow iliyokabidhiwa
kwa katibu wa bunge imekutwa inasambazwa mitaani huku ikiwa imenyofolewa
kurasa tatu za mwisho zenye majina ya waliohusika na mgawo wa fedha
hizo kwa lengo la kutengeneza propaganda ili kuwadanganya wananchi kuwa
taarifa hizo hazijawataja wahusika.
Akizungumza na waandishi wa habari mwenyekiti mwenza wa ukawa Mh. James
Mbatia amesema zipo taarifa za baadhi ya waliokuwa wanasambaza taarifa
hizo kuwa wamekamatwa na jeshi la polisi na kuwataka wananchi kutoa
taarifa kituo cha polisi ili waweze kuchukuliwa hatua haraka ambapo
amesesistiza kwamba (UKAWA) wanataka taarifa hiyo iwasilishwe bungeni
kwa ajili ya kujadiliwa Jumatatu .
ITV imemtafuta kamanda wa polisi mkoa wa dodoma David Misime na katibu
wa bunge Dr.Thomas Kashilillah ambao wamesema nao wanazisikia taarifa
hizo na wanazifanyia kazi ili kutoa taarifa yao.
Chanzo: ITV